Loading...
 

Utambulisho wa Kuwa Mshauri

 

 

Kuwa Mshauri ni Nini?


Kuwa mshauri ni mchakato ambapo wanachama wenye ujuzi wanatoa muda wao, umakini, maarifa, mwongozo, ufahamu, na ushauri. Kwa wanachama wapya, hii inawasaidia kwenye mwanzo wao ndani ya Agora. Kwao, dunia ya Agora inaweza kuwa inaogopesha sana, na wanaweza wasijue wapi kwa kuanza au jinsi ya kuingia kwenye jamii. Washauri wanatoa mwongozo kwenye maeneo makuu manne:

  • Jukwaa la Agora -  Wanawasaidia wanachama wapya kujiongoza kwenye mifumo tofauti ya Agora - maongezi, majukwaa, kurasa za mitandao ya kijamii, usimamizi wa klabu, nk.
     
  • Utamaduni wa Klabu - Kuwaelezea wanachama wapya jinsi klabu inavyofanya kazi, vipengele maalum vya kitamaduni na desturi ambavyo vipo, jinsi ya kuomba msaada, jinsi ya kujiunga kufanya majukumu. Wanawatambulisha wanachama wapya kwa shughuli za kijamii zisizo za Agora (kwa mfano, uanazuoni, sherehe, shughuli), nk.
     
  • Mpango wa Kielimu wa Agora - Jinsi muundo wa mpango wa kielimu ulivyo, wapi kwa kupata miradi ya kielimu, jinsi ya kufanya majukumu tofauti kwa usahihi, kutoa ushauri kwenye miradi ya kwanza.
     
  • Jamii ya Agora ya Duniani kote - Jinsi klabu inavyojumuishwa kwenye jamii ya Agora ya duniani kote, mashindano na matukio mbalimbali ya klabu ambazo zipo, taarifa za makongamo ya kikanda na ya kimataifa, nk.
     
  • Kumsaidia mwanachama mpya kufanikisha malengo yake maalum ndani ya klabu.

 

Kwanini uwe Mshauri?

Kuwa mshauri ni moja ya mbinu zenye ufanisi mkubwa wa kujifunza ujuzi kwa muda mfupi.

Kulingana na Sir Ken Robinson (Mwandishi, mzungumzaji, na mshauri wa kimataifa wa Kiingereza wa elimu ya sanaa kwa serikali, mashirika yasiyo ya kibiashara, elimu, na taasisi za sanaa), kuwa mshauri kuna majuu manne ya kimsingi:

Kutambua - ‘Washauri wanatambua cheche ya shauku au furaha na inaweza kumsaidia mtu kuchambua vipengele maalum vya eneo ambalo linaendana na uwezo na shauku ya mtu huyo…

Kutia moyo - ‘Washauri wanaweza kutuongoza kuamini kuwa tunaweza kufanikisha kitu ambacho kilionekana hakiwezekani kwetu kabla hatujakutana nao. Hawaturuhusu kushindwa kujiamini kwa muda mrefu au kwamba ndoto zetu ni kubwa sana. Wapo kutukumbusha kuhusu ujuzi ambao tayari tunao na ni nini tunaweza kukifanikisha tukiendelea kufanya kazi kwa bidii…

Kuongoza -‘Washauri wanaweza kusaidia kutuongoza… kwa kutupa ushauri na mbinu, kututengenezea njia, na hata kujikwaa kidogo wakati wapo pembeni yetu ili kutusaidia kupona na kujifunza kutoka makosa yetu…

Kunyoosha - ‘Washauri wafanisi wanatusukuma kupita kile ambacho tunaona ni kikomo chetu. Kama vile wanavyotukataza kuwa tusijiamini, wanatuzuia pia kufanya vitu vichache iwezekanavyo na maisha yetu. Mshauri wa kweli anatukumbusha kuwa lengo letu daima halitakiwi kuwa 'wastani' katika kutafuta kwetu…

Mshauri:

  • Ameshapitia njia ambayo wewe unaanza - wanajua nini kinafanya kazi na kipi hakifanyi kazi. Wameshafanya makosa ambayo unaweza kujifunza bila maumivu ya kupitia hayo mwenyewe.
     
  • Wameshatengeneza mtandao wa mawasiliano. Hii ni muhimu haswa kama unachagua mshauri wa mradi wako wa jamii. Mshauri anaweza kukutambulisha kwa baadhi ya watu muhimu ambao wanaweza kufungua milango kwako.
     
  • Atakusukuma ubaki kwenye njia na kuwa thabiti, kuunda tabia.
     
  • Aataongeza kwa kiwango kikubwa nafasi yako ya mafanikio.
     
  • Atakupa ushauri wa kiuaminifu na usio na ubaguzi kuhusu hotuba yako au mradi. Kwasababu haumlipi mshauri kitu chochote, hakudai chochote na anaweza kuwa wazi na vitu ambavyo anaviona sio.

Contributors to this page: zahra.ak and agora .
Page last modified on Sunday August 15, 2021 12:44:37 CEST by zahra.ak.